U Mawazoni

17 06 2009

Masika yamepita,

Mawazo hayajaisha,

Hata macho nikiyafumba…

Bado nakutazama,

Hata kichwa vipi nikilikuna…

Bado nakuwaza,

U mawazoni n.m.


Actions

Information

6 responses

17 06 2009
yasinta

Dada Serina umesema,
mawazo yapo daima,
tena daima na daima,
mpaka kichwa chauma,
na kufikiri u´kichaaa
mawazo.

17 06 2009
Fadhy Mtanga

u mawazoni usiku na mchana…..
umeutawala moyo kwa sana….
u mawazoni nirudie tena….
sababu mi nakupenda sana….
ni wewe mwinginewe sijamwona…

17 06 2009
ringojr

Sasa serina jamni MASIKU ndio nini?

17 06 2009
Serina

Asanteni nyote kwa maoni yenu… Luihamu, habari ya masiku?

29 06 2009
Kissima

Jua lachomoza, mpaka linazama,
bado nazidi kukuwaza,
maumivu nayasikia,
katika moyo yanavyokata,
sugu chapitiliza kidonda,
kamwe sijutii kupenda,
ipo siku nitakupata,
kila ninachotaka,
hakika nitakipata.

2 07 2009
Bwaya

Umuwazaye sana

…Eni Emu

Kwa heshima na taadhima

…Eni Emu?

Pasi shaka ushaelewa hitaji langu

…Eni Emu?

Leave a comment