Naamka na tabasamu,
Maana najua wewe ni wangu,
Hisia zinazonipitia kwangu,
Furaha tupu, mwenzangu!
Napendelea unavyonipapasa…
Kwa maneno zilizo na ladha,
Natikirinywa na lako tabasamu…
Ujuzi ushaigundua wa kunipa hamu,
Na kumbatio lako mwenzangu…
Humtuliza shetani wa kiume wangu!
Huyu shetani wangu wa kiume…
Amejua nani ndie mme,
Keshawafukuza wengi nakwambia …
Kila umbo kutoka kila daraja,
Maskini, tajiri, vijana , wazee,
Warefu, wafupi, weusi na weupe,
Lakini sasa naamka na tabasamu…
Na sio maneno tu hunifanya,
Nikalala na tabasamu…
Umeniweza!


Hi!
Good to see you’re back
This seems to explain a lot as to your disappearing act LOL as you say, kweli amekuweza haha and I wish you a life full of tabasamus
Just had to read this again.
Kumbe una shetani wa kiume? That’s an excuse I may start using soon as well! I thought it was just your temperment
Ama kweli amekuweza!
Shetani wako amekumaliza!
serina,
kuwezwa na amekuweza ni maneno mawili tofauti.
kuweza ni kwakipindi kilichopita na amekuweza ni kwakipindi kilichopo
who knows about kesho kama atakuweza? au wewe ndio utamuweza au yeyote watawezana.
Changamoto tu Serina.
amani.
DUH!
@ Ria: Thanks! I actually believed it was a severe case of PMS
@ Mwanasosholojia: Shetani wangu amenisaidia kuchuja!
@ Ras Lui: Naishi kwa ya leo… na kwa leo, ananiweza
@ Simon: DUH! maanake nini?
duh!!! makubwa.
Umeniweza vile navotaka,
Hakika leo sina tena mashaka,
Niwapo nawe siishi kuburudika,
Napata nguvu hata nihisipo kuchoka,
Umeniweza hadi mtima kusisimka,
Kila uchao nazidi kuhamanika,
Umeniweza!
Ni nyongeza tu da Serina.
@ Fadhy: Asante kwa nyongeza!
@Serina : Duh! maana yake ni DUH!:-)
You are tagged. Visit mine for details and comply.
Bomseh…noted.