05.05.09
Umeniweza…
Naamka na tabasamu,
Maana najua wewe ni wangu,
Hisia zinazonipitia kwangu,
Furaha tupu, mwenzangu!
Napendelea unavyonipapasa…
Kwa maneno zilizo na ladha,
Natikirinywa na lako tabasamu…
Ujuzi ushaigundua wa kunipa hamu,
Na kumbatio lako mwenzangu…
Humtuliza shetani wa kiume wangu!
Huyu shetani wangu wa kiume…
Amejua nani ndie mme,
Keshawafukuza wengi nakwambia …
Kila umbo kutoka kila daraja,
Maskini, tajiri, vijana , wazee,
Warefu, wafupi, weusi na weupe,
Lakini sasa naamka na tabasamu…
Na sio maneno tu hunifanya,
Nikalala na tabasamu…
Umeniweza!


Ria said,
May 5, 2009 at 17:32
Hi!
Good to see you’re back
This seems to explain a lot as to your disappearing act LOL as you say, kweli amekuweza haha and I wish you a life full of tabasamus
Ria said,
May 5, 2009 at 17:41
Just had to read this again.
Kumbe una shetani wa kiume? That’s an excuse I may start using soon as well! I thought it was just your temperment
Mwanasosholojia said,
May 6, 2009 at 03:45
Ama kweli amekuweza!
Shetani wako amekumaliza!
ringojr said,
May 6, 2009 at 06:28
serina,
kuwezwa na amekuweza ni maneno mawili tofauti.
kuweza ni kwakipindi kilichopita na amekuweza ni kwakipindi kilichopo
who knows about kesho kama atakuweza? au wewe ndio utamuweza au yeyote watawezana.
Changamoto tu Serina.
amani.
Simon Kitururu said,
May 6, 2009 at 06:50
DUH!
Serina said,
May 6, 2009 at 09:24
@ Ria: Thanks! I actually believed it was a severe case of PMS
@ Mwanasosholojia: Shetani wangu amenisaidia kuchuja!
@ Ras Lui: Naishi kwa ya leo… na kwa leo, ananiweza
@ Simon: DUH! maanake nini?
ringojr said,
May 6, 2009 at 11:02
duh!!! makubwa.
Fadhy Mtanga said,
May 6, 2009 at 16:53
Umeniweza vile navotaka,
Hakika leo sina tena mashaka,
Niwapo nawe siishi kuburudika,
Napata nguvu hata nihisipo kuchoka,
Umeniweza hadi mtima kusisimka,
Kila uchao nazidi kuhamanika,
Umeniweza!
Ni nyongeza tu da Serina.
Serina said,
May 6, 2009 at 19:31
@ Fadhy: Asante kwa nyongeza!
Simon Kitururu said,
May 8, 2009 at 10:47
@Serina : Duh! maana yake ni DUH!:-)
bomseh said,
May 8, 2009 at 11:09
You are tagged. Visit mine for details and comply.
Serina said,
May 11, 2009 at 09:12
Bomseh…noted.