Sawa, tuendelee kidogo… “Robot, Polyamory na Chura”

14 05 2009

Niliamua kuitika mwito wa Bomseh na kuwafunulia kidogo maisha ya Serina. Nawashukuru kwa maoni yenu na nim’amua kuendeleza kidogo tu!

Kwa kunitembelea hapa nawaona kama ndugu zangu na pia naamini duniani hakuna siri, ingawa sote twapenda kujistiri kwa kuyafunga midomo yetu.

Wachache wenu m’meandika kuhusu hotuba zinazotolewa kwenye matanga, yangu sitaki iwe mistari inayosimua historia yangu… kaenda shule sijui wapi, alipenda ushairi, amewaacha wanaume kadhaa na watoto kadhaa…. la hasha, sitaki. Sitaki hotuba ya aina yoyote… Maisha yangu na kazi zangu nataka zijizungumuzie.

Nimefurahia kujua kuwa kati yenu kuna wanaume wasioogopa kuingia jikoni na pia kusaidia katika shughuli nyumbani. Kama mwanamke, binti, mama, dada … nawashukuru kwa hilo maana wanawake tumezoea kuvumilia mengi maana hatutaki kuonekana wavivu. Na ninaomba tafadhali muwasaidie wenzenu na shughuli nyumbani hata kama mnawalipa, kazi ya nyumba huwa haiishi na hata akina yaya, boi, ‘robot’ na waajiriwa wengine wote ni binadamu, na huchoka. Uliza mwafrika aliyeishi ughaibuni na hana starehe za wafanyikazi nyumbani…

Tuendelee na swala la “Polyamory” … sijui tafsiri yake kwa kiswahili ni ipi … waswahili mpo?

Huwa na keti na kuwaza sana kuhusu mila na desturi zinazopatikana kotekote duniani. Hili wazo la ‘Polyamory’ lilijitokeza baada ya kutazama filamu moja ya kimaasai, shughuli za kuchoma mkuki mlangoni, na pia kwa kusikia visa vya kina mama na mazubeda maishani mwao… mwamkumbuka Zubeda?

Sidhani kuna chochote kibaya na uhusiano wa wazi kati ya watu wazima ilmradi wajikinge kutokana na magonjwa ya zinaa na pia waweke wivu kuleeee mpakani kule. Mwenzangu kwa mfano akitaka kuwa na mke wa pili, bora awe na sababu halisi, siwezi mkataza… amini usiamini! Naamini ya kuwa ” there is always enough love to go around ” … au? Labda nilisheruka kichwa na sijajitambua :D

Kaka Bwaya naye aliulizia ‘profile ya a good frog‘ . Kwanza neno frog nililitumia sio kutokana na umbo la chura bali nilikumbuka hadithi ya ‘The princess and the frog’ na pia filamu ya Shrek. Huwa natazama sana filamu za watoto (mazoea).

Kabla sijaandika kuhusu chura wangu, ningependa kuwakumbusha ya kuwa Penzi halilazimishwi ni mtu kwa mtu wake au Marazz alivyojibu, kila jini na mbuyu wake.

Mwenzangu tumefahamiana mda mrefu. Tulikutana hukuhuku nilipo sasa lakini njia zetu zikaenda panda. Alirudi nyumbani Afrika nami nilibaki huku. Hatukujua kuwa pepo zingeturusha pamoja tena.

Ni mtu mwenye upendo sana na mvumilivu kupita kiasi. Mcheshi. Hanioni tu kama mwenzake lakini pia kama mtu binafsi. Kama Serina.

Kuna vitu vingi ninavyoona anapozungumuza na watu wa kila aina, mimi, marafiki na hata familia. Ana heshima. Mkarimu. Mungwana kweli… Hana kiburi… ningependa kuendelea lakini machozi yananilenga machoni…

Weekendi njema!





Honest scrap award á la Serina

11 05 2009

Thanks a heap Bomseh for this toturous exercise… what more could a woman wish for? It is an honour to be requested to share what makes me tick with all of you… I do count somewhere on this planet after all :D

Before you read this, some of the information may be a deemed as inappropriate but hey, I was asked for honesty.

scrap-award

I wanted to make it something poetic but that has already been done here . But all in all, maybe there are a couple of things or more people would be shocked to learn about me… not that that’s what I’d put here. Ok, now that I’m obliged to comply…

The Catch

You must brag about the award

You must include the name of the blogger who bestowed the award on you and link back to the blogger

You must choose a minimum of seven (7) blogs that you find brilliant in content or design.

Show their names and links and leave a comment informing them that they were prized with Honest Weblog.

List at least ten (10) honest things about yourself. Then pass it on with the instructions

One honest thing before I start, I never pass on chain letters, nor read them… but this was FUN.

1. Househelp

I work just as hard around my home as I do when visiting home. I cannot tolerate people who give the househelps a to do list by the minute. ” Auntie, hebu njoo nikutume dukani…kisha pitia dhobi uniletee nguo zangu…kabla hujaondoka, watoto wako wapi? wamekula? Sawa, kimbia urudi kisha upanguze ukuta kabla wageni hawajafika…..blah,blah,blah” How these wonderful women stick to their jobs I wonder. All the househelps I’ve come across think I’m crazy when I chip in and do some work while all the other mamas just sit and piga mdomo…kwani one can’t talk while working…and we wonder why the hubbies stray…ahem.

2. Maisha na soko

I love going to open air markets wherever in the world regardless of hali ya hewa. In nairobi, I’m addicted to Gikomba and Marikiti markets… just the thrill of watching masses move and the mkokoteni guys who never fail to test my agility. City market bores me but what fascinates me up to date is that no matter how shoddily I dress, the guys always run towards me saing ” Sista, CHANGE, DOLLARS” …how do they sniff me out?

I also remember when I was expecting my daughter, I’d get this craving for properly fermented Uji from mama kibuyu… not this supermarket ready concotions but proper Uji fermented with patience….the only place I realized I could get some of this without slaving in the kitchen was at Gikomba and the fishmongers there that entertained me with their stories in between serving their customers while i sipped my uji in the most comfy chair cuishoned specially for me by them… yes, there are kind souls even in eastlands…became my friends to date.

3. Asti moments

Anybody who has been through my FB profile will tell you exactly how many Asti moments I write about. Naongea kuhusu Cinzano Asti. This is the one drink I’ve come to enjoy and drink ocassionaly at my own pleasure and leisure. But one thing Asti does to me is that it makes me so mellow that all I want to do is dance on the table. So if any of you desires a table dance…just show up with a bottle of Asti…LOL.

4.Homepubs

I’m not a very social human being as may have been marked by how many blogs I frequently visit but never leave comments and neither am I a guzzler, but I do love a cold Pili now and then when at home and in good company. The home pub or Grocery inavyojulikana nchi jirani always offers an interesting place to catch up on whats going on and who’s been up to what when one has been away for a while. I’m always there with my favourite sister and some of our childhood pals. We have left clubbing to the yo-yo’s of these days and it isn’t funny bumping into your nephews and nieces when gyrating to zilizopendwa. The only place they dare not step till they are 30+ is the home pub. The blogging world is a lot like my local-pub I should say. It’s enough kuketi na kusoma.

5. Research

This will be the death of me. I have always been a curious soul and love to find solutions. My latest Hypothesis is that the world won’t end if I call it quits with books. There are times it gets so frustrating that I think I’d be happier being a housewife since I work just as hard at home as any househelp I have ever met anyway…. so why am I toturing myself trying to do it all? This calls for meditation… kwa hivyo nikipotea hapa sana…msishangae.

6. Polyamory

This ONLY happens a lot in my dreams. Lakini si mwajua…ndoto ni ndoto…. Maybe I should have been born in the days of Solomon.

7. Of the Stars and men

Intrestingly enough, I have only been in long term relationships with Tauruses and Leos… so there are times like now when I get Birthday reminders every other day. Not that I totally believe in stars lakini vitu vingine there’s is no other way of explaining them. Being a cardinal Water sign, I’m supposed to cope well with the bull … but that is what a bull is… a BULL. On the other hand, a relationship with a leo requires a lot of balance, they will either dehydrate me (being a fire sign) or I’ll drench them out…hehe… I’ve perfected the balance and we just simmer… which beats being lukewarm any day hands down. And as you know with the Simba, anavyozidi kuzeeka, ndivyo ujuzi wake wa kunguruma na kuuma huzidi…jijazie.

8. Make and spend.

I find it hard to be a miser/freeloader. I spend to satisfy my whims and those of my near and dear if I can afford it and they are not freeloading on me… I know these are the people who’ll spread my ashes or carry my geneza when I die if I do die before them, and probably shed a tear or two while at it. I have no qualms whatsoever with people spending their money as they wish but a pennypinching man has never made it to my good books. I get put off by men who can brag about all their assets and yet put their families on stringent daily budgets… just to squander the spoils on whatever it is they do outside the house.

9. Men in the kitchen

I have had the priviledge of being cooked for by men without the expectation of getting kitu kidogo afterwards and this to me is one of the best ways to get my attention. It proves that the men would go out of their way to make me comfortable and it was more flattering than getting a diamond studded necklace that you would only wear once a year. Talk of instant gratification.

10.  the love of my life

… that’s an entire new story… i’ve had to go through many frogs to get this one…and just like in Shrek, if he is really a frog, he’s a good one.

There are many of you who write splendid content on your blogs and it is my duty to give you your 15 seconds of fame…hehe… najua wengine wenu mliandika mda uliopita lakini binadamu hubadilika na wakati kwa hivyo raundi ya pili tafadhali.

Luihamu

James Adolwa

Marvin Tumbo (even after your exams…)

Yasinta

Mubelwa

Bwaya

Fadhy

Mwanasosholojia

Kissima

Simon





Umeniweza…

5 05 2009

Naamka na tabasamu,

Maana najua wewe ni wangu,

Hisia zinazonipitia kwangu,

Furaha tupu, mwenzangu!

Napendelea unavyonipapasa…

Kwa maneno zilizo na ladha,

Natikirinywa na lako tabasamu…

Ujuzi ushaigundua wa kunipa hamu,

Na kumbatio lako mwenzangu…

Humtuliza shetani wa kiume wangu!

Huyu shetani wangu wa kiume…

Amejua nani ndie mme,

Keshawafukuza wengi nakwambia …

Kila umbo kutoka kila daraja,

Maskini, tajiri, vijana , wazee,

Warefu, wafupi, weusi na weupe,

Lakini sasa naamka na tabasamu…

Na sio maneno tu hunifanya,

Nikalala na tabasamu…

Umeniweza!