Tembea, tembea…

29 04 2009

Tembea, tembea usichoke…

Tembea uone dunia,

Uyaone ya ulimwengu

Tembea ufuate riziki,

Tembea ukawaone marafiki,

Tembe, tembea…

utafute pesa,

utafute mali,

utafute amani,

utafute penzi,

utafute unachotaka kutafuta.

uridishe moyo wako…

hujafungwa pingu,

hujakalishwa kitako…

Tembea, tembea…

Tembea uende shughulini,

mapato lazima siku hizi,

Nenda sokoni, dukani,

zilizobaki pitishia

‘grocery’ na kisha nyumbani

Tembea, tembea…

Kiguu na njia…

Tembea na nia.


Actions

Information

13 responses

29 04 2009
Subi

ama kwa hakika “Mwenda bure si sawa na mkaa bure”, tembea uone!

29 04 2009
ringojr

MAKUBWA!!!DUH

Lakini Serina kuna wale wanaolala na kuletewa.

1 05 2009
ringojr

serina siku hizi uko busy sana,kwani tenzi zimepungua sana si kawaida yako au?

Duh !!

2 05 2009
Serina

@ Subi, Karibu.
@Luihamu, wajua maisha bwana….

2 05 2009
Kaasa

Nice. My motto: Tembea.

4 05 2009
Fadhy Mtanga

Tembea wala usichoke,
Kokote kule ufike,
Riziki yako uidake,
Nyumbani waridhike,
Tembea, tembea.

4 05 2009
Serina

@Kaasa, Wise girl :D .
@ Fadhy, Karibu.

4 05 2009
Mwanasosholojia

Serina malenga wetu
Unagusa mioyo yetu
Kuzisoma akili zetu
Kuzirusha beti kwetu

Nami nipo matembezini
Natembea hapa duniani
Kwa sasa nipo masomoni
Nchi ya watu ughaibuni

Hii yote ni kutembea
Vitabu kuvisomea
Nyumbani bongo kurejea
Taifa letu kujengea

Nakukaribisha buloguni
Wala sikuweki kapuni
Sitakutupa asilani
Wewe kwangu ni fanani!

4 05 2009
Kissima

Tembea tembea,
kijiweni nimejikuta,
kwa Serina nachangia.
siku zilipita,
mashairi hatukuyapata.
sasa nayafurahia,
kimoyomoyo najiimbia.

Kwa nini kuhadithiwa,
tembea utajionea.

5 05 2009
Serina

@ Mwanasosholojia na Kissima, karibuni na asante.

5 05 2009
Bwaya

Bora umerudi Serina…

Rudi bloguni…

5 05 2009
Ria

“Kiguu na njia…
Tembea na nia.”

Thanks for the advice!

6 05 2009
Serina

@ Bwaya: Asante

@ Ria: Don’t take it personally.

Leave a comment