Shughuli hapa na pale zaniita…
Kuzitimiza bila malalamiko desturi,
Ulegevu huu umetoka wapi?
Maungo kwa machofu nimevunjika,
kama mganga anayepunga pepo kilingeni…
Mwisho wa simba umeletwa na nzi!
.
Hapa nasema, pale nakimya…
Jogoo la shamba haliwiki mjini…
Ongeza kasi, jua latua…
Huu ni uvivu wa kike au ni balaa?
Maliza ya leo, leo… ya kesho mageni
Hivi kumbuka walipwa masaa
Lakini tena…
Sheria hazitii wasiwasi aliyetosheka!
Nimetosheka.



Kutokuridhika ndiyo ya mwanadamu asili
Ukishiba sasa njaa itakupa akili
Ili kesho na ule kufanza mzunguko kamili
Utoshekapo fikiri
Hujatosheka utagundua
Kwani kutokutosheka ndiyo asili
umetosheka?
hajatosheka…
najikwamua kwa leo
najituma kwa/ya leo
nitajitahidi kwa leo
pochi,mshiko,midikodiko
jah ahsante.
amani.
“Mwisho wa simba umeletwa na nzi”
That is a mighty good line…
Nimejaribu kuandika kama wenzio hapa juu lakini Kiswahili imegonga ukuta.
How’s that?
Great Poem…
Regards
Umenikumbusha wahindi wanaoajiri wafanyikazi nyumbani kwao kisha kuwaambia wachambue vitunguu saumu karibu gunia nzima kila wiki baada ya kazi ya nyumbani.Vituko vyao nilipata kujua kutoka msichana anayenisaidia kazi nyumbani kwangu sasa. Eti kila saa ilikuwa, harakisha, harakisha, sitakulipa kuketi nde!
@ Bwaya: kweli: lakini kugundua saa zingine hutokea kiajali
@ Ras Lui: Maisha hayo… kuna, ukunwe.
@ Marvin: Nendelea hivyo hivyo… hatua moja ikifuatwa na nyingine.
@Ria: Ukoloni mambo leo (Neocolonism)!
[...] a poem called ‘Nimetosheka‘ (I am fed up) she says, Shughuli hapa na pale zaniita… Kuzitimiza bila malalamiko desturi, [...]