Maisha Safari

17 03 2008

Kitoto kichanga…

Hukaribishwa na wengi,

‘kishezaliwa tu! safari huanza!

kuishi duniani mkondo wa kwanza.

Wengine safari, kwao huwa fupi…

waliobakia nao mola awanusuru!

kulingana na sheria za wengine ataishi

Hawezi chagua…

mlezi wake duniani,

Hawezi chagua…

kati ya ukafiri na dini.

Amri zifuatwe bila ubishi!

Sio wote hubahatika…Safari hii kuimaliza.

Wengine safari huwa fupi…

wengine ndefu…

wengine safari ya furaha…

wengine safari ya matatizo.

Kisha baleghe…

Uamuzi mikononi mwake…

atakavyoishi ye…

na wengine wanaouhusiano naye,

atakavyofanya ye…

atakavyojitetea jangwani.

Wengine wana safari ngumu…

iliyojaa majaribio na mahangaiko,

Wengine safari, starehe tupu!

Waishije maisha yako?

Wanungunika?

Watesa?

Wateseka?

Wayafurahia?

Kufa…

wengine hujipangia…

wengine hupangiwa…

Kaka husema,

Kuzaliwa bahati…

Kufa lazima.

Nd’o maisha hayo!





Maiko*

3 03 2008

Leo nauvunja mtindo wangu wa mashairi maanake naandika kumhusu Maiko wangu ambaye ni mmoja wa watu wa kwanza kuyasoma mashairi yangu nilipokuwa bado kijana. Na nikishesoma kuhusu akina Stela na wengine wengi…wacha nami nimwage mtama kwenye kuku. Read the rest of this entry »