Kimya

21 12 2007

Kukimya kwangu…

sio kumaanisha sina la kusema

maoni sitaki tu kutema

macho zaidi yan’tazama

Kukimya kwangu…

sio kumaanisha maneno sina

hotuba si neno geni ni tabia

moyoni hata hivyo najiimbia

Kukimya kwangu…

sio kuwa wa kusema nae sina

usifikirie kuwa ni ujinga

na tena ujue sio kuringa

Kukimya kwangu…

sio kumaanisha sijui nitamke vipi

bado sijafungwa ulimi

macho nayo bado usingizi

Kukimya kwangu…

ni njia ya kujifunza tena nakwambia

masikio niliyojaliwa yanapata kusikia

walio na lakunena nafasi nawapatia

Kukimya kwangu…

najua ni unyonge wangu

na pia ni nguvu kwangu

hilo lako jibu mwenzangu

Kukimya kwangu…

ni kusema kwangu.