Rafiki

24 10 2007

Rafiki…

narudia neno hili

polepole

nikionja utamu wake

n’natabasamu peke yangu

kwani najua kuwa

rafiki huyu…

ni rafiki wa kweli

milango mingi tum’pitia

madirisha vilevile

um’nisaidia kukusanya kamba zangu

na kuzifuma pamoja

mkeka um’pendeza

bila we rafiki

sijui ungefanana aje.

Rafiki…

n’natabasamu kwani

husiti

kuniambia ukweli ulivyo

yawe machungu

au

yawe matamu

na cha muhimu kabisa

wanipa sikio lako

iwe kwa dakika chache

au masaa kabambe

Rafiki…

washangilia nami

mazuri yanapotokea

na kuniliwaza

n’napopatwa na mazito

Rafiki…

nakupenda.





Asubuhi ya leo

23 10 2007

Asubuhi ya leo

nimeshuhudia ajali

Mwanamke kagongwa na gari

Alikuwa amepotea mawazoni

Aitazama simu

Badala ya kutazama aendako

Breki hizo!

Kilio hicho!

Sitasahau maishani mwangu…

Asubuhi ya leo

N’nafurahia kuishi

Kupumua

Kupenda

Sina malalamiko

kumbuka

Asubuhi ya leo

ni wengi

hawajaiona.





Upumbavu

4 10 2007

Mbona wanipasua moyo?

Kila dakika upo mawazoni…

Chochote nifanyacho,

nafanya kukufurahisha…

Mbona waniotesha ndoto

hadi mtindo unakuwa glasi moja kila siku?

La sivyo usingizi haunipati….

Mbona wanipandisha joto

kisha kunimwagia maji ya baridi?

Mbona ukanyemelea kwenye panya hili

Na kunifanya nikupende kikumbavu?

Mbona ubavuni kuna

Nafasi isiyojazika?

Lengo lako ushanieleza,

Najua wanitaka…

au wanitania?

Nami nakutaka…

Au nabahatisha?

Lakini

Mbona mambo ya dunia

magumu hivi?

Sisi sote wapumbavu sio?

Twajua tutokapo, hatujui tu tuendako.