In’bidi niandike tena
Vitu nane wataka kujua
Vitu nane nit’watambulia
Nimalizapo mi’ kusema
Zamu nanyi m’tapewa
Vitabu ni la kwanza,
hunionyesha mwangaza
Pili, napenda upekee
lakini sio upweke
Kujivunia upishi wangu namba tatu
kuridhisha wengine raha yangu
Nne, marafiki nawathamini
Bado sijajua ni kwa nini
Tano, useremala nim’jaribu
mbao nim’pasua bila aibu
Hata hivyo mazingira nayajali
namba sita sio kwa ajali
Nafasi ya saba naipa ndoto
maisha mazuri kwa wote watoto
La nane mjaze wenyewe
au tuseme tu ni uzembe
Watu nane … zamu yenu
Ndesanjo (sio zile za Ethan…zingine)
na nane mkishewachagua
msisahau pia kuwajulisha


Serina , haka kashughuli kweli !:-)
this is the first blog i’ve read in swa. will be back for more
@ Simon: shughuli si kitu kizuri?
@ kipusa: karibu.
Serina you caught me unawareness,it was like shaggy with his song IT WASNT ME,
Nilibaki nikicheka tu,na kushangaa
hongera,Serina unakumbuka mchezo wa SHAKE,NADHANI SHAKE NA TAGGED ni brain challenge.
Hehe finally managed to get my list up! Thanks for the tag!
[...] kuandikiwa na Serina nikiambiwa niainishe vitu nane kuhusu [...]