N’natumaini

24 01 2007

Kam’ kawaida,

kuwaza na kuwazua…..

nini kipya wauliza?

sina mapya…

matumaini tu!

N’natumaini kuwa u nuru yangu,

Utanionyesha njia wakati wa giza

Utanionyesha mbele n’napofika mwisho

Utaniliwaza n’naposhikwa na msiba

N’natumaini kuwa hutan’peleka mrama,

hata kam’ tum’gombana,

hata kam’ tum’koseana,

hata kam’ tun’ maswala ya kindani

yanayosababisha mapambano.

N’natumaini kuwa hut’nipa kamba,

un’ambie n’ende zangu.

Nim’pokea kamba nyingi maishani mwangu,

n’lizorundika kwenye sitoo,

nafikiria kushona mkeka

n’tauweka kwenye shoo.

N’natumaini matumaini yangu,

Hayat’kupa unyonge…