uchaguzi kidemokrasia…
yu wepi tuliyemchagua’si?
demokrasia yapeleka nchi mbele…
mafunzo ya wakoloni tushazoea,
bila demokrasia msaada ham’tapokea,
wafuateni wajuao njia msijepotea!
mwasema tuithamini demokrasia…
madawa hospitalini twasubiri,
msingi kwa vijana mliahidi,
barabara vijijini zafika lini?
endesha pajero demokrasia…
petroli gari wajaziwa,
nyumba kodi walipiwa,
masikini naye an’angalia!
lala hotelini demokrasia…
chokora si tatizo langu ’sha kwambia,
kazi yako si ulijichagulia?
niambie kingine kisicho gasia.
umoja ni nguvu twajivunia…
kura zenu mlinipa uhakika gani?
sie nyie mwajiita wapinzani?
mbona mwanililia’mi? Jameni!
majimbo kidemokrasia…
msiukaribie mpaka wetu!
msijichanganye na wakwetu!
msinitatize na shida zenu!!
kama demokrasia wapishe walioteuliwa….
wanichochea bahati haikuwa yako,
uchaguzi ujao labda zamu yako,
si demokrasia kwa wote?